Saturday, February 28, 2009

Na Kenneth Mwazembe
Tunduma

Kundi la vijana wenye hasira kali zilizochochewa na mkuu wa kituo cha polisi mjini Tunduma A.S. Wendo wamevamia nyumba ya diwani wa kata ya Tunduma na ambaye pia ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi Aden Mwakyonde na kuvunja vioo 83 vya madirisha 14 na kuwajeruhi mgambo wanne.

Chanzo cha ghasia hizo ni kukamatwa kwa baiskeli za vijana hao zilizokuwa zikitumika kuvusha mahindi na mchele mpakani mwa Tanzania na Zambia kwa madai kuwa ni operesheni usafi wa mji.

Vijana hao wamesema kuwa polisi walianza ukamataji wa baiskeli hizo usiku wa Februari 26 na kuendelea 27 ambapo vijana hao wamedai kuwa wamedaiwa fedha (RUSHWA) ili kukomboa baiskeli hizo.

Katika kukabiliana na kitendo hicho ambacho wamekiita unyanyasaji unaofanywa na jeshi hilo vijana hao waliandamana kuelekea kituo cha polisi ili kuishinikiza polisi kuwarejeshea baiskeli zao ambapo mkuu wa kituo aliwaambia waende kuchukua baiskeli hizo kwa diwani wao.

Kauli hiyo ndiyo iliyowafanya wao kurusha mawe kituoni hapo na baadaye kwenda nyumbani kwa diwani wao na kuharibu madirisha yote na kuipiga mawe nyumba hiyo.

Akizungumza na gazeti hili Aden Mwakyonde alieleza kuwa alipigiwa simu na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi shirikishi ya mjini hapa kuwa kuna maandamano makubwa ya vijana wenye hasira wakienda nyumbani kwake hali iliyomfanya awapigie askari polisi.

“Nimepiga simu kwa OCS ili atume askari kuzuia madhara ambayo yangeweza kutokea lakini hakufanya hivyo, alidai hana gari, mke wangu amempelekea magari mawili akadai hawawezi kutumia salon wanataka gari la wazi hata alipopelekewa gari la wazi akasema ni chakavu kasha akaondoka kwenda mjini Vwawa” alilalama Mwakyonde.

“Nimewaomba polisi wawape vijana hao baiskeli zao ili kuepusha shari ambayo ingeweza kutokea lakini polisi hawakufanya hivyo na hivyo kunisababishia hasara hii ”aliongeza Mwakyonde akielekeza lawama zote kwa jeshi la polisi.

Mwenyekiti huyo aliyekua akihudhuria kikao cha kamati ya uchumi na mipango alilazimika kuacha kikao na kukimbilia nyumbani kwake akiwabeba mkuu wa polisi wilayani hapa Stephen Mtengeth na timu yake lakini alipofika na kuona nyumba imeharibiwa aliwajia juu na kuwafukuza OCD na timu yake ya watu wane.

Hatua hiyo na ambayo imewaudhi polisi hao imelalamikiwa vikali kutolewa na kiongozi kama yeye wakidai angetumia busara.

Mkuu wa kituo cha polisi cha Tunduma aliyejitaja kwa jina moja la A. S. Wendo alipohojiwa juu ya yeye kuwa chanzo cha ghasia hizo alikanusha na kudai kuwa yeye amewatuliza wakakataa na hivyo kumfanya aende wilayani kuomba msaada wa askari wengine.

“Niliamuru kupigwa kwa mabomu ya machozi ili kukinusuru kituo baada ya vijana hao kutaka kukivamia” anaongeza Wendo.

Mamlaka ya mji mdogo wa Tunduma inafanya operesheni ya kusafisha mji kwa kuondoa uchafu katika mifereji na vibanda vya wafanyabiashara ndogondogo ambayo ilianza juzi ikahamia na kukamata baiskeli hali iliyozusha machafuko yaliyosababisha wanamgambo wa halmashauri wane kujeruhiwa na mmoja kulazwa katika hospitali ya wilaya ya Mbozi mjini Vwawa.

Mgambo waliojeruhiwa ni John Mwakalinga ambaye amelazwa katika hospitali ya Vwawa na Andrew Sing’ambi aliyetibiwa na kuondoka na wengine wawili ambao hawakuweza kupatikana majina yao .

Muuguzi katika wodi la majeruhi Ester Nyondo ameeleza kuwa hali ya mgonjwa huyo inaendelea vizuri.

Hili ni tukio la tatu tangu mwaka 2006 ambapo ghasia za mpakani zilizuka kufuatia kifo cha Lukas Msuya kuuawa katika mahabusu za Zambia lile la mgomo wa mawakala wa usafirishaji (Clearing & Forwarding) ambapo katika ghasia hizo kulitokea uharibifu wa mali na majeruhi.

Mkuu wa wilaya ya Mbozi Halima Kihemba alipohojiwa juu ya matukio hayo alikiri kupewa taarifa muda mchache uliopita na kwamba kwa wakati huo alikuwa safarini Tukuyu kwenye kikao.

Wednesday, February 18, 2009

Mchungaji Cosmas Mwasenga (48) aliyekamatwa na viungo vya binadamu anayedaiwa kuwa albino siyo mchungaji kitaaluma, imefahamika.

Kukamatwa kwa mchungaji huyo na ambaye alidaiwa kuwa ni kanisa la Pentekoste kumewastusha wakuu wa madhehebu hayo ambao walidai kuwa hawana mchungaji wa jina hilo.

Askofu wa kanisa la Muungano wa Makanisa ya Kipentekoste wilayani Mbozi Erasto Makalla akizungumza na gazeti hili amesema kuwa, mtu huyo kabla hajabadili tabia alikuwa ni muumini wa kawaida wa madhehebu hayo ya Pentecoste Holiness Mission (PHM), na kuwa alikuwa akiwahubiria watu waokoke wamjue Yesu.

“Tumefuatilia kujua mchungaji aliyehusika na tukio hilo na tumeambiwa sio mchungaji kama ilivyoelezwa, ila kutokana na uwezo wake wa kuwashuhudia watu ili wapate wokovu, walimpa jina la Mchungaji, lakini yeye siyo mchungaji bali kazi yake ni mhunzi” alisema Askofu Makalla.

Makala aliongeza kuwa Umoja wa makanisa hayo unaendelea kufuatilia ili kujua habari zaidi za mtu huyo (anayedaiwa kuwa mchungaji), baada ya hapo watatoa taarifa rasmi.

Mwenyekiti wa kijiji cha Nambala Jumanne Mziho aliyewaongoza askari kupekua nyumba ya Luseshelo Mwashilindi alisema kuwa Februari 13 saa 11 za jioni Polisi walifika kilabuni na kumtaka awaongoze nyumbani kwa Mwashilindi.

Polisi huyo aliyejitambulisha kwa jina la Inspekta Ndimbo akiongozana na E.276 D/Sgt Datstan na F. 679 D/Sgt Daniel wakiwa na watuhumiwa Cosmas Mwasenga na Luseshelo Mwashilindi walifanya upekuzi na kukuta Mifupa miwili inayosadikika kuwa ya binadamu, na chupa 18 za dawa aina ya Benzyl Penicillin na maji ya kuyeyushia dawa hiyo chupa 14, na koti jeusi la Mchungaji, vitu ambavyo vilikutwa bafuni kwa Luseshelo.

Mziho aliendelea kueleza kuwa baada ya polisi kuona mifupa hiyo waliwahoji watuhumiwa kueleza juu ya mifupa hiyo ambapo Mwashilindi alisema ni mifupa ya mzungu hali Mwasenga akisema ni ya Albino.

Imeelezwa kuwa siku mbili kabla ya tukio watuhumiwa hao walikwenda Mbeya katika maeneo ya Mwanjelwa wakitafuta mteja wa kununua mifupa ya kunguru mweupe, jambo ambalo lilifanya wasamaria wema kutoa taarifa Polisi ambao waliweka mtego ambao ulipelekea kukamatwa kwa watu hao.

Afisa Tarafa wa Tarafa ya Iyula Nathian Mpandachombo alipoulizwa kama kuna tukio lolote la kifo cha albino katika eneo lake alithibitisha kuwa hakuna mtu yeyote wa aina hiyo aliyepotea kwani idadi ya walemavu wa ngozi waliopo katika tarafa yake wote wapo.

Tuki linalofanana na hilo liliwahi kutokea katika kijiji cha Mpanda kata ya Nyimbili ambapo mwananchi mmoja ilidaiwa alifukua kaburi alilokuwa amezikwa albino ambaye alikuwa nduguye wa familia moja kisha kukimbilia wilayani Chunya ambako kuna machimbo ya dhahabu, lakini baadaye Polisi walidai kuwa kaburi hilo lilikuwa limefukilwa nusu tu na kwamba walithibitisha kuwepo kwa mifupa hiyo.
MWISHO.

WALIOMPIGA IMAMU WAPANDA KIZIMBANI

Posted by Unknown On 5:52 AM No comments
Na Kenneth Mwazembe
Mbozi

Watu wawili wamefikishwa katika mahakama ya Wilaya ya Mbozi kwa tuhuma za kumpiga Imamu wa msikiti wa Ijumaa mjini Tunduma Husein Issa Baluza (32) akiwa anaswalisha sala ya alasiri.

Watuhumiwa hao ndugu, wametajwa kuwa ni,Thabit Ismail 37 mkazi wa mji mdogo wa Tunduma na Nasoro Ismail (28) mwanafunzi wa chuo kikuu kishiriki cha Muhimbili .

Ilidaiwa mahakamani hapo na mwendesha mashitaka wa polisi Cyprian Michiria kuwa manamo tarehe 16 Februari mwaka huu kwa pamoja watuhumiwa hao walimshambulia kwa kumnyoshea vidole na kumjeruhi usoni na kumchania shati lake lenye thamani ya shilingi 10,000.

Washitakiwa wote wawili wamekana shitaka mbele ya hakimu Enock Matembele na kesi imeahirishwa hadi tarehe 18 Machi ambapo itatajwa tena na washitakiwa wako nje kwa dhamana ya shilingi laki tano kila mmoja.

Wakati huo huo jeshi la polisi wilayani hapa limeimarisha ulinzi katika msikiti huo baada ya kugundua kuwa waumini wa msikiti huo wamegawanyika makundi mawili la kwanza likimshabikia imamu Husein Issa anayeungwa mkono na Bakwata na lingine likimuunga mkono mwalimu wa madrasa Ahmed Pongwa.

THE PASTOR'S STORY INTERESTED MANY

Posted by Unknown On 5:42 AM No comments
The story of the pastor who got 6 months imprisonment as found in this blog interested many people including Mr. Mark who has been encouraging me. Heredown the story as translated by Mr. Mark a blogger who came in Tanzania in 2004 to study Mbozi local language and Kiswahili the main language of East Africa people.

Tanzanian Pastor faces 6 months in prison after refusing to swear on BibleSaturday 7 February 2009 by Mark
I’d always wondered how Jesus’ instructions to his followers not to swear on any thing, but to let their “yes be yes, and no be no” applied to swearing on the Bible in court. So I was fascinated to hear this tale of a Tanzanian pastor. It’s told by Kenneth Mwazembe, and is in Swahili, so the quoted text below is my translation:
Pastor of the EAGT [Evangelical Assemblies of God in Tanzania - a large Pentecostal denomination] church on Ichenjezya street in the town of Vwawa, Mbozi District of Mbeya Region, Simon Kitwike (48), yesterday found himself with a 6 month jail sentence for contempt of court after refusing to swear the witness oath because of his religious faith.
The Pastor who had had his house broken into at the end of last year and had some things stolen, arrived at Mbozi District court to give his witness but refused to swear, claiming that it would be wrong.
The District Judge Kajanja Nyasige commanded him to read the section of the Bible which tells him not to swear in court, so the Pastor opened the Bible and read Matthew 5:35, which is where his view comes from.
… Judge Nyasige continued to be patient with the Pastor in order that he have the chance to change his stance, by commanding him to read from the Bible again - from the letter of Paul to the Romans 13:1-5. The witness read this section in front of the court, but when he was asked if he had changed his stance, he replied that he was unable to change his stance from this verse, and insisted that his position was still the same.
Judge Nyasige was compelled to read him the judgement that he was guilty of contempt of court and so was sentenced to go to jail for 6 months, and also that he would be expected to give his testimony in the original case on March 2nd this year. read more
What would you have done were you the judge? The judge was quite right in saying that Paul tells the church in Romans 13:1-5 that they should submit to the government and those in authority, but what happens when the law of the country directly contradicts an instruction of Jesus?
It’s an interesting dilemma that could equally have happened in the UK (and maybe has done in the past?) and highlights the irony of laws that require witnesses to swear on a book which instructs people not to swear on anything but simply let their yes be yes and their no be no.
Tags: , , , , , , , Posted in Africa, Church, Swahili, Tanzania 1 Comment »

Friday, February 6, 2009

Baada ya miaka mingi ya mahangaiko ya kukosa mawasiliano katika kijiji cha Ntinga sasa waanza kunufaika na kivuko kilichojengwa kwa msaada wa mradi wa TASAF II.



hivyo ndivyo walivyonaswa na kamera zetu
Mchungaji Simon Kitwike aliyehukumiwa kifungo cha miezi sita jela kwa kosa la kukataa kuapa mahakamani ameeleza kuwa haikuwa nia yake kukataa kuapa bali aliiomba mahakama atoe ushahidi bila kuapa.

Aliyasema hayo jana nyumbani kwake alipozungumza na Tanzania Daima mara baada ya kutoka gerezani ambako amefungwa kifungo cha nje, alielezea mkasa uliompata Oktoba 25 mwaka jana saa 6 za usiku alipovamiwa na kundi la majambazi lililovunja mlango wa nyumba yake na kuwaamuru kutoa fedha.

Kitwike alitaja mali zilizoibiwa kuwa ni pamoja na fedha taslim shilingi milioni 1,212,000, godoro moja, seti moja ya luninga, radio mbili, rewinder moja, masanduku mawili yaliyokuwa na nguo za mchungaji huyo na simu za mkononi mbili vyote jumla vikiwa na thamani ya shilingi milioni 2.2.

Baada ya majambazi hao kuondoka mchungaji alipiga kelele za kuomba msaada ambapo majirani walifika na kuanza msako ambao ulifanikiwa kuwanasa watuhumiwa watatu akiwemo mwanamke mmoja aliyekutwa na redio ambaye alipohojiwa alimtaja mumewe kuwa ndiye aliyempa redio hiyo, mtuhumiwa ambaye hadi hivi sasa hakamatwa pamoja na polisi kuarifiwa.

Kuhusu tukio la yeye kufungwa mahakamani Februari 4 mwaka huu, Kitwike amesema kuwa hakukataa kuapa kwa kusudi bali aliiomba mahakama imruhusu kutoa ushahidi wake bila kuapa kwa kutumia kifungu katika Biblia Mathayo 5:33-37 ambacho kinasema “Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa usiape uongo ila mtimizie Bwana nyapo zako lakini mimi nawaambia usiape kabisa hata kwa mbingu kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu”

Hakimu Nyasije Kajanja kabla hajatoa hukumu alimwamuru mchungaji huyo kusoma Waraka wa Warumi 13:1-2 kinachoeleza kuwa “Kila mtu na aitii mamlaka iliyokuu kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu, na ile iliyopo imeamriwa na Mungu, hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu nao washindanao hujipatia hukumu”

Ndipo Hakimu huyo alimsomea kifungu cha sheria na 198 (1) kama ilivyorekebishwa mwaka 2002 kinachokataza mtu kudharau Mahakama na kuwa kuendelea kukataa kuapa ni kuvunja sheria na hivyo anatenda kosa la jinai.

Ndipo hakimu alipomhukumu kwenda jela miezi sita kwani sheria inasema asiyeapa ametenda kosa la kudharau mahakama ambalo adhabu yake ni kifungo cha miezi 12 jela, hata hivyo kufuatia utetezi alioutoa mahakamani hapo hakimu aliamua kumfunga kifungo cha miezi sita gerezani.

MTOTO ERICA APATA MSAADA

Posted by Unknown On 8:35 AM No comments
Watanzania wawili wanawake wanaoishi Marekani wametoa msaada wa dola 200 za Marekani kugharamia matibabu ya mtoto Erica Laurent (1) aliyekataliwa na baba yake baada ya kuzaliwa bila njia ya haja kubwa.

Wanawake hao Elizabeth Sawe wa Dallas na Joyce Joseph wa California waliamua kumsaidia mtoto huyo baada ya kusoma habari za Erica na kuona picha yake katika blogu ya http://www.maishanivita.blogspot.com/ ambayo ilimuonesha mtoto huyo akiishi matumbo yakiwa nje.

Mtoto huyo aliyezaliwa Novemba 2007 na Huruma Mwaijande akiwa na tatizo la kutokuwa na njia ya haja kubwa alikuwa akitibiwa katika hospitali ya rufaa mjini Mbeya ambapo walimfanyia upasuaji wa awali uliosababisha eneo la kitovu alipopasuliwa kufumuka mara baada ya ushonaji hali iliyowalazimu waganga hao kumshauri mama wa mtoto kuendelea kumlea hadi atakapofikia umri wa mwaka mmoja ndipo upasuaji ufanyike.

Kutokana na hali ya umaskini wa kutisha unaoikabili familia hiyo mume aliamua kumtekelekeza mkewe na kumwacha akihangaika ambapo alilazimika kuomba msaada wa wasamaria.

Wasamaria hao katika ujumbe wao wamesema kuwa haja yao ni mtoto Erica kupewa matibabu yanayostahili na kukua kama watoto wengine.

Wametoa wito pia kwa Watanzania wengine kuwasaidia wenye shida kama mtoto huyo “Tunaomba watu wawe na huruma na moyo wa kusaidiana kwani ukimsaidia mtoto kama Erica ambaye ni malaika unakuwa umejiwekea hazina mbinguni, Erica ni malaika ambaye hajui kitu duniani” ilisema sehemu ya ujumbe huo.

Hivi sasa mtoto huyo yuko katika hospitali ya Peramiho ambapo anatarajiwa kufanyiwa upasuaji Februari 9 mwaka huu.
Na Kenneth Mwazembe
Mbozi.

Wananchi 95 wakazi wa kijiji cha Nambala Wilayani Mbozi mkoani Mbeya juzi waliandamana hadi kituo kikuu cha Polisi kulishinikiza Jeshi la Polisi Wilayani hapa kuwaachia huru wana kijiji wenzao wanne waliowekwa mahabusu na jeshi hilo.

Jeshi hilo liliwakamata watuhumiwa hao kwa kosa la kupekua nyumba ya Penson Nkoswe na kubomoa nyumba za wanakijiji wenzao kinyume cha sheria.

Mwenyekiti wa Kijiji hicho Jumanne Mziho aliwataja watu waliokamatwa na ambao wamekuja kudai waachiwe kuwa ni Moses Nzunda (36), Julius Mwashilindi (51), Wadi Mwashilindi (42) na Tomaso Nzunda (30) ambao wanatarajiwa kupandishwa kizimbani kujibu tuhuma hizo.

Mziho aliongoza maandamano hayo hadi kumwona Kamanda wa Polisi wilayani hapa ambaye alitumia busara kumaliza mgogoro huo baada ya kuwasikiliza na kufanya mazungumzo baina yake na viongozi wa kijiji na kata yaliyofanya polisi kusalimu amri na kuwaachia kwa dhamana.

“Sisi tumekuja kudai haki na kutaka kufahamishwa kama Jeshi letu limeacha mpango wa Ulinzi Shirikishi na badala yake kuzitumia taarifa za watu wenye chuki dhidi ya mpango huo, na kuwatia nguvuni wananchi wasio kuwa na hatia” alisema mwenyekiti.

Alisema tatizo lililopo kijijini kwake ni la mwanakijiji Penson Nkoswe ambaye amekuwa akipinga juhudi zinazo fanywa na kijiji hicho za kuimarisha ulinzi na usalama dhidi ya wahalifu sugu ambao wamekuwa wakijificha na kulindwa na Nkoswe.

Naye mwenyekiti wa kamati ya ulinzi wa kijiji hicho Tadeo Nzunda alibainisha kwa kuwa taja wahalifu wanaolindwa na Nkoswe kuwa ni Luka Mgode (31), Jelas Sampamba (29) na Mpandachilima Mwasaka (22) ambao hujihusisha na mtandao wa wizi wa mifugo, baiskeli, redio na Tv.

Nzunda alisema Januari 27, mwaka huu watuhumiwa waliiba ng’ombe mmoja wa Wilson Shombe (56), na wengine wawili mali ya Ibrahim Chelelo na Beledon Nzyela ambapo wanakijiji walipofanya msako walimkamata Luka Mgode nyumbani kwa Nkoswe akiwa na ng’ombe mmoja na wenzake walifaulu kutoroka.

“Kitendo hicho kilipandisha jazba kwa wanakijiji ambao kwa idhini ya mkuu wa kituo cha Polisi kilichojirani mjini Mlowo, alitoa idhini kufamya upekuzi na kuwasaka wahalifu katika nyumba ya Nkoswe wakati baadhi yao wakiwa na hasira kali walivamia nyumba za washukiwa na kuziharibu nyumba zao” alisema.

Hata hivyo watuhumiwa waliokuwa rumande waliachiwa kwa masharti ambayo hayakuweza kufahamika maramoja jambo ambalo liliwafanya wenzao waliokuwa nje kidogo ya eneo la Polisi kuanza kuimba nyimbo za kuashiria ushindi dhidi ya kitendo hicho.

Nkoswe alipotakiwa kujibu tuhuma zilizoelekezwa dhidi yake alikanusha na kudai kuwa hahusiki na lolote ingawaje alikubali kuwa na mahusiano ya karibu na Sampamba ambaye alimtetea kuwa ni mtu mwema.

Mwanakijiji Menard Msongole ameeleza kuwa nyumba moja mali ya Leward Nzunda imechomwa moto na watu wasiofahamika tukio linaloleta wasiwasi kuwa linahusishwa na uhasama uliojitokeza kati ya wanakijiji wema na wanaotuhumiwa wa uhalifu kijijini hapo.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya Zerothe Stephen alipotakiwa kuzungumzia tukio hilo kwa njia ya simu kutoka Mbozi alisema bado hajapokea taarifa kutoka eneo la tukio hilo.

Uchunguzi zaidi umebaini kuwepo kwa kukamiana hali itakayohatarisha amani kutokana na walifu kulipiza kisasi kwa kuchoma nyumba huku wanakijiji wema wakidai kuwa watachukua hatua mikononi mwao mara watakapowatia mikononi mwao kwani wamechoshwa na vitendo hivyo.

Jeshi la polisi mkoani hapa litahitaji kuchukua hatua za tahadhari kabla hali haijawa mbaya kwani wananchi wana wasiwasi na jeshi hilo kutokuwa serious.
mwisho

Thursday, February 5, 2009

MCHUNGAJI WA EAGT AFUNGWA JELA MIEZI 6

Posted by Unknown On 11:09 PM 1 comment
Mchungaji wa Kanisa la EAGT lillilopo mtaa wa Ichenjezya mjini Vwawa wilayani Mbozi mkoani Mbeya Simon Kitwike (48) jana alijikuta akihukumiwa kifungo cha miezi sita gerezani, baada ya kudharau mahakama kwa kukataa kuapa ili atoe ushahidi kutokana na imani ya Dini.

Mchungaji huyo aliyevunjiwa nyumba yake mwishoni mwa mwaka jana na kuibiwa mali kadhaa za nyumbani kwake alifika katika mahakama ya wilaya ya Mbozi ili kutoa ushahidi wake, lakini alikataa kuapa kabla ya kutoa ushahidi wake akidai ni dhambi.

Hakimu wa mahakama ya wilaya Kajanja Nyasige alimwamuru asome kifungu katika Biblia kinachomtaka asiape mahakamani, ndipo mchungaji huyo alifungua Biblia na kusoma kitabu cha Mathayo 5: 35 kuwa ndicho kinachompa msimamo huo.

Baada ya kusoma kifungu hicho Hakimu Nyasige alimuuliza tena mshitakiwa (shahidi) kama atakuwa tayari kuapa ili aweze kuendelea na kutoa ushahidi wake mahakamani, hata hivyo mshitakiwa huyo aliendelea kubaki na msimamo wake wa kukataa kuapa.

Ndipo Hakimu huyo alimsomea kifungu cha sheria na 198 (1) kama ilivyorekebishwa mwaka 2002 kinachokataza mtu kudharau Mahakama na kuwa kuendelea kukataa kuapa ni kuvunja sheria na hivyo anatenda kosa la jinai.

Hata hivyo hakimu Nyasige aliendelea kumvumilia mchungaji huyo ili aweze kubadili msimamo wake kwa kumwamuru asome Biblia hiyo tena Waraka wa Mtume Paulo kwa Warumi 13:1- 5, shahidi huyo alisoma kifungu hicho mbele ya mahakama, lakini alipoulizwa kama amebadili msimamo wake alijibu kuwa hawezi kubadili msimamo wake, kwa aya hiyo ya waraka na akasisitiza kuwa msimamo upo pale pale.

Hakimu Nyasige alilazimika kumsomea hukumu na kumtia hatiani kutokana na kosa la kuidharau mahakama, hivyo anamhukumu kwenda jera miezi sita na kuwa atatakiwa kuja kutoa ushahidi wake kwa kesi ya msingi Marchi 2, mwaka huu.

Mwandishi wa habari hizi alimhoji Mchungaji mwandamizi wa Kanisa hilo aliyejitaja kwa jina moja la Mwakasaka ambaye alisema amesikitishwa na hukumu hiyo na akadai kuwa mchungaji wake alielewa vibaya vifungu vya biblia vinavyozungumzia viapo.

Naye Mchungaji Erasto Makalla wa kanisa la Pentekoste alieleza kusikitishwa kwake na hatua hiyo ya mchungaji kupingana na mamlaka ya serikali na akasema kuna haja ya kuwafanyia semina wachungaji ili waelewe taratibu za serikali.

Matukio ya upinzani yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara wilayani hapa ambapo mwaka juzi waumini wa madhehebu ya Mashahidi wa Jehova walikuwa kwenye mgogoro na serikali baada ya kukataza wanafunzi wasiimbe wimbo wa taifa na kuheshimu bendera.

mwisho.

Site search

    More Text