Wednesday, February 18, 2009

WALIOMPIGA IMAMU WAPANDA KIZIMBANI

Posted by Unknown On 5:52 AM No comments
Na Kenneth Mwazembe
Mbozi

Watu wawili wamefikishwa katika mahakama ya Wilaya ya Mbozi kwa tuhuma za kumpiga Imamu wa msikiti wa Ijumaa mjini Tunduma Husein Issa Baluza (32) akiwa anaswalisha sala ya alasiri.

Watuhumiwa hao ndugu, wametajwa kuwa ni,Thabit Ismail 37 mkazi wa mji mdogo wa Tunduma na Nasoro Ismail (28) mwanafunzi wa chuo kikuu kishiriki cha Muhimbili .

Ilidaiwa mahakamani hapo na mwendesha mashitaka wa polisi Cyprian Michiria kuwa manamo tarehe 16 Februari mwaka huu kwa pamoja watuhumiwa hao walimshambulia kwa kumnyoshea vidole na kumjeruhi usoni na kumchania shati lake lenye thamani ya shilingi 10,000.

Washitakiwa wote wawili wamekana shitaka mbele ya hakimu Enock Matembele na kesi imeahirishwa hadi tarehe 18 Machi ambapo itatajwa tena na washitakiwa wako nje kwa dhamana ya shilingi laki tano kila mmoja.

Wakati huo huo jeshi la polisi wilayani hapa limeimarisha ulinzi katika msikiti huo baada ya kugundua kuwa waumini wa msikiti huo wamegawanyika makundi mawili la kwanza likimshabikia imamu Husein Issa anayeungwa mkono na Bakwata na lingine likimuunga mkono mwalimu wa madrasa Ahmed Pongwa.

0 comments:

Post a Comment

Thank you for reading the article

Site search

    More Text