Monday, September 1, 2014

Ugugaji kuku wa kienyeji

Posted by Unknown On 1:50 AM No comments
Ufugaji kuku na hasa wa kienyeji ndiyo njia pekee ya kumkomboa mwananchi vijijini kiuchumi. Serikali inapaswa kuhakikisha madawa ya mifugo na kinga au chanjo inayouzwa madukani iwe halisi na ya ukweli isiwe kama mwaka 2013 chanjo feki ilizagaa madukani matokeo yake wafugaji waliochanja mifugo yao ilikufa. Nani amefanya tahmini ya hasara iliyowafika wakulima hao? Nani anawalipa fidia ilihali mkulima ni kama mtoto yatima ambaye hapaswi kudeka?
 Ufugaji wa kuku ukienda sanjali na ukulima utanufaishana kwani kuku watapata mazao ya kilimo nalo shamba litarutubishwa na mbolea ya kuku.
Mzunguko huo wa mazao na mifugo mwaisho wa siku utakuwa na tija
 Hivi ndivyo tunavyofuga, hapa chini ni wenzetu wa Ethiopia wanafuga kisasa ambacho tuliowengi hatuwezi kutokana na gharama za mtaji zinazohitajika.
 Banda hili linatufaa kwa wale wenye maeneo ya kati yaani lenye ghorofa ili kuwa na nafasi kubwa ya kufugia ambapo unaweza kufuga huria hayo mabanda wakatumia kulala na kutagia.
 Kwa wale wa mijini unaweza weka banda kama hili uwani na ukafuga bila matata

0 comments:

Post a Comment

Thank you for reading the article

Site search

    More Text