Saturday, September 20, 2014

NFRA kununua tani 200,000 za mahindi

Posted by Unknown On 7:06 AM No comments
Ununuzi wa mahindi ulioanza wiki iliyopita utapunguza kwa sehemu kubwa ukosefu wa soko uliojitokeza kwa msimu huu 2014/15 ambapo wakulima waliuza kwa wafanyabiashara kwa shilingi 24,000 kwa plastic kilo 20 badala ya shilingi 500 kwa kilo inayotolewa na Wakala wa Hifadhi ya Chakula ya Taifa.

Licha ya ununuzi huo serikali inapaswa kubuni shirika litakalofanya biashara ya ununuzi na usagaji wa nafaka ili hata maamuzi ya kuuza mahindi nje yasiwepo tuuze unga yaani ni mahindi yaliyoongezwa thamani.

Pamoja na hayo changamoto ni nyingi ikiwepo uchache wa vituo vya kununulia mahindi hayo hali inayosababisha mlundikano mkubwa wa magari na kulazimu magari kukaa wiki bila kushusha mzigo.

Wiki iliyopita Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Godfrey Zambi alisema serikali imepanga kununua jumla ya tani 200,000 bila kueleza umma kuwa hizo tani 200,000 ni kati ya tani ngapi zilizozalishwa na kwa kiasi hicho amewasaidiaje wakulima ambao kwa vyovyote wamezalisha zaidi kuliko uwezo wa serikali kununua.
 Hilo ni lundo la mahindi yaliyonunuliwa  kwa wiki moja

 Ustadi wa kazi unatukumbusha enzi za Shirika la Usagishaji la Taifa yaani NMC

 HUo ni upimaji unaoendelea hivi sasa

Mijadala inaendelea kwa madereva waliokaa hapo kwa zaidi ya wiki bila kushusha mahindi

0 comments:

Post a Comment

Thank you for reading the article

Site search

    More Text