Saturday, September 20, 2014

Posted by Unknown On 7:25 AM No comments
Barabara kuu ya Dar es Salaam - Lusaka Zambia maarufu kwa jina la Tanzam Highway eneo la Songwe kwa Feston linaharibika baada ya wananchi wa eneo hilo kufungulia maji ya mfereji na kufanya bwawa kando ya barabara bila kuelewa madhara yake.

Mhandisi wa Tanroad mkoa wa Mbeya James Nyakabari hajaona hilo. Pia maeneo mengi kuanzia Tunduma hadi Mlowo yameharibiwa na mifugo, wenda kwa miguu na magari yanayochepuka na hivyo kula mabega ya barabara (Road shoulders) zaidi ya mita 2.

Ukarabati wa mara kwa mara unahitajika ili kuziba nyufa badala ya kungoja kujenga kuta.

Hii ndiyo hali halisi ya bwawa hilo kando ya Tanzam Highway kwenye kizuizi cha ukaguzi ushuru wa mazao


Maji yakitiririka toka kwenye mfereji wa umwagiliaji na kuingia kando ya barabara ya lami


 Ndoo zinazotumika kuchotea maji kwa ajili ya kuoshea magari na pikipiki


0 comments:

Post a Comment

Thank you for reading the article

Site search

    More Text