Thursday, November 19, 2009

Watumishi watano wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi wamepandishwa kizimbani kujitu tuhuma za wizi wa vocha za pembejeo zenye thamani ya shilingi milioni 86.

Watumishi hao ni Joseph Mbogela (59) afisa kilimo, Asante Ndimbo (46) afisa kilimo na Tekla Luoga (54), wengine ni Maiko Mwashiuya (45) dereva, Goodluck Mbazu (33) dereva na Richard Mnkondya (41) mfanyabiashara aliyepatikana na vocha mali ya wizi zenye thamani ya shilingi milioni 25.

Watuhumiwa wote ambao walishitakiwa mbele ya hakimu wa mahakama ya wilaya Nyasige Kajanja wamekana mashitaka yaliyosomwa dhidi yao na mwendesha mashitaka wa polisi Charles Makunja.

Kesi itatajwa tena Disemba 5, washitakiwa wamepewa dhamana ya maneno ya shilingi milioni 5.

0 comments:

Post a Comment

Thank you for reading the article

Site search

    More Text