Tuesday, August 5, 2014

Nanenane 2014 Kilimo ni Biashara

Posted by Unknown On 12:09 PM No comments
Maonesho ya kilimo, mifugo na ujasiriamali ni fursa pekee inayoonesha hisia za watanzania kuhusu matarajio yao kulinganisha na fursa zilizopo.

Watunga sera wamekuwa wakiwayumbisha wakulima kwa kutoa sera zisizotekelezeka na porojo nyingi. Ilipobuniwa kaulimbiu ya Kilimo kwanza wengi walikuwa na tumaini ya kuushinda umaskini wakidhani serikali ingekuja na mikakati kabambe ya utekelezaji wa kilimo kwanza kwa vitendo kumbe sivyo ilivyotokea.

Maenesho ya nanenane jijini Mbeya yamefana licha ya kukumbana na changamoto kadha wa kadha zinazojitokeza. Tumaini la wakulima walio wengi walitarajia sera imara zingewekwa ili kuwa na fursa kwa vyombo vya fedha kuchangia moja kwa moja katika kilimo.

serikali ibuni mikakati ya kuwakopesha wakulima hawa wadogo wajishughulishe na ujasiriamali utakaohusisha usindikaji wa mazao yao na kuyauza vizuri.

Kati ya mambo yaliyochekesha mwaka huu ni pale serikali inapojitangaza na kujigamba kuwa itaiuzia shehena ya mahindi Kenya takriban tani 50000, Tujiulize kuwa fursa iliyokuwepo inapotea kwa kuuza ghafi bila kusindika na kuyaongezea thamani huo ni upwagu.


Hilo ndiyo banda la maonesho la jiji la Mbeya linasema Kilimo ni Biashara.

Hilo ni kati ya mabanda machache yaliyoandaliwa

Hiyo ni bustani ya jiko imewekwa hapo kama shamba darasa kwa mtu asiye na eneo unaweza kufanya hivyo

0 comments:

Post a Comment

Thank you for reading the article

Site search

    More Text