Tuesday, August 5, 2014

Wakulima kazi kwelikweli

Posted by Unknown On 12:36 PM No comments

Pamoja na jitihada zinazofanywa na mkulima mmoja mmoja za kuzalisha mazao ya kilimo chakula na biashara bado mazingira yake ni magumu analima bila kuwa na uhakika wa soko. Bei zenyewe zinapangwa na wanunuzi halafu sisi wa mjini tunalaumu ughali wa chakula kumbe ni wanunuzi wa kati ndiyo wanalangua mazao hayo. Serikali iandae vema mazingira ya kuwa na soko la uhakika kupitia mamlaka zake au hata vyama vya wakulima (vikundi). 
Ushirika uliotarajia kusaidia kutatua matatizo ya soko leo hii ushirika ni marehemu na bila kutafuta chombo mbadala hali itaendelea kuwa mbaya. Serikali itenge fedha za ununuzi wa mazao yote na kuelekeza nguvu kama sera inavyotamka.

Serikali ikishindwa kumtafutia mkulima soko la mazao yake itawalazimu kudai kwa nguvu kwani mkulima hana likizo yaani sawa na yatima kwani yatima hadeki.


Mambo yalivyokuwa katika uwanja wa nanenane wa John Mwakangale juu ni vifaranga wa Malawi chini ni mkulima wa Tunduru akiwa katika banda lake akionesha muhogo babu kubwa.

Hapo juu ni madumu ya asali ya nyuki wakubwa ba wadogo karibuni

Maonesho haya hayakuacha kuonesha kuku kama ndege wa kukupa kipato na anaweza kufugwa na kaya maskini.
Hao kuku ni aina ya Kenya wanaitwa Kenbro Dr Mbwaga wa Uyole ndiye mfugaji wa kuku hao

0 comments:

Post a Comment

Thank you for reading the article

Site search

    More Text