Thursday, June 5, 2008

Na Kenneth Mwazembe
Mbozi

Chama cha Mapinduzi wilayani Mbozi mkoani Mbeya kimetoa sh 50 elfu na salaam za pole kwa wachezaji wa timu ya mpira ya Chipaka Rangers ya mjini Tunduma kufuatia ajali iliyotokea jana katika eneo la Tunduma iliyojeruhi watu 16.

Katibu wa CCM wilaya ya Mbozi Aluu Segamba aliyefika katika hospitali ya wilaya kuwaona majeruhi, ameeleza kusikitishwa kwake na ajali hiyo ambayo imewafanya baadhi ya wachezaji kuvunjika viungo vyao na kwamba chama kipo pamoja nao katika wakati huu mgumu wa kuuguza majeraha.

Mganga Mkuu wa hospitali ya wilaya Egifrid Mwingirihela amewataja majeruhi 10 ambao wamepelekwa hospitali ya rufaa kutokana na hali zao kuwa mbaya ni Manase Siwelwe, Joseph Simumba, Rogers Siwale, Sultan Simumba, Jacob Sikaonga, Yona Sikanyika, Leonard Sinkala, Ruben Sinkala, John Siwale, na Aron Sikaonga

Wengine ni Alick Siame, Timoth Siame, Paulo Siwelwe, Izukanji Sikaonga, Antony Simwinga na Imasi Silungwe ambao ameeleza kuwa hali zao zinaendelea vizuri na wanapata matibabu katika hospitali yake.

Akisimulia ajali ilivyotokea, majeruhi Alick Siame (48) anasema kuwa dreva aliyekuwa anaendesha gari Mitsubishi Fuso lenye namba za usajili T160 ARG (Jina la dreva halikupatikana) kuwa alikuwa akiendesha kwa mwendo kasi hali iliyomfanya ashindwe kulidhibiti na kupinduka.

Gari hilo lilibeba wachezaji na washabiki wa mpira waliotoka kucheza mechi mjini Tunduma wakirejea kijiji cha Chipaka ambapo gari liliacha njia na kupinduka.

MWISHO

0 comments:

Post a Comment

Thank you for reading the article

Site search

    More Text