Tuesday, May 20, 2008

Na Kenneth Mwazembe
Mbozi MAJAMBAZI

Watu wawili wanaodhaniwa kuwa majambazi wameuawa kwa kuchomwa moto na wananchi katika kijiji cha Chimbuya wilayani Mbozi mkoani Mbeya.

Afisa Mtendaji wa kijiji hicho Alfred Siwale amewataja waliouawa kuwa ni Ruben Mbukwa (52) mkazi wa kijiji cha Ukwile na mwingine aliyejulikana kwa jina moja la Shibanda mkazi wa Tunduma.

Siwale ameeleza kuwa mnamo Mei 18 mwaka huu majambazi wapato 7 walivamia duka la Aswile Kibona na kuiba bidhaa zote na kisha kutokomea ambapo usiku wa pili walirudi tena na kuvunja nyumba alimokuwa amelala na kumjeruhi kwa risasi na mapanga ambapo haijajulikana kama walipata kiasi chochote cha fedha.

Wezi hao kabla hawajaanza unyama huo walifunga milango ya majirani kwa nje na kisha kupiga hewani risasi nne kuwatisha waliotaka kutoa msaada na baadaye kutoroka ambapo wananchi waliamua kufanya msako uliowakamata watu 7.

Mmoja wa waliouawa Ruben Mbukwa alikutwa na risasi moja ya shotgun iliyoamsha hasira za wananchi na kumpa kipigo na baadaye moto.

Polisi waliofika kijijini hapo wamefaulu kuwakamata Mafikiri Sinkala (34), mkazi wa kijiji cha Mpemba, Mwinyi Nyilu (25), Alex Msukwa (25), Majuto Mwamgunda (17), Victor Mwembe (23) wote wakazi wa Ukwile.

Majeruhi Aswile Kibona amekimbizwa katika hospitali ya rufaa ya mjini Mbeya kutokana na majeraha ya risasi aliyopata.

Jeshi la Polisi wilayani hapa limethibitisha kutokea tukio hilo na kwamba uchunguzi unaendelea ambapo bado hawajaipata silaha aina ya shotgun iliyotumika katika uhalifu huo.

MWISHO

Saturday, May 10, 2008

SIKU YA WAUGUZI DUNIANI

Posted by Unknown On 4:31 AM No comments
Na Kenneth Mwazembe
Mbozi

Sherehe za maadhimisho ya kumbukumbu ya muasisi wa fani ya Uuguzi duniani Florence Nightngale zitafanyika kesho kimkoa katika wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya.

Akizungumza na gazeti hili jana ofisini kwake Afisa Muuguzi hospitali ya wilaya ya Mbozi Michael Abdi amesema wataadhimisha kumbukumbu hiyo kwa kumuenzi Florence Nightngale kwa kuwasha mishumaa mawodini, kuwatembelea wagonjwa na kutoa zawadi.

Ameeleza kuwa wilaya imejiandaa kupokea wageni 500, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Mbeya John Mwakipesile anatarajiwa kuwa mgeni rasmi. Sherehe hizi zinatarajiwa kuhudhuriwa na wakuu wa wilaya zote nane na Wakurugenzi wa Halmashauri zote za mkoa huu pamoja na Waganga wakuu wote wa hospitali.

Abdi meendelea kueleza kuwa wauguzi wanaadhimisha siku hiyo wakiwa bado wanayo matatizo kadhaa katika fani hiyo ikiwamo mishahara midogo isiyolingana na majukumu yao, kilio cha posho ya mazingira hatarishi na uchache wa vyuo vya wauguzi ambapo uchache wa wauguzi unawafanya waliopo kufanya kazi kwa zaidi ya masaa stahili bila kulipwa posho.

Maadhimisho ya sikukuu hiyo ambayo hufanyika kila mwaka Mei 12 ni kumkumbuka muanzilishi wa fani ya uuguzi duniani Florence Nightngale aliyezaliwa mwaka 1820 na kufariki 1910 ambapo alifanya kazi katika mazingira magumu akitumia mishumaa na taa za kandili wakati wa usiku.

Kwa mujibu wa afisa huyo sherehe hizo zitapambwa kwa vikundi vya ngoma toka Nambinzo Mawazo Tulyanje, Mang’oma toka Msanyila, kwaya mbili za wauguzi wenyewe na kikundi cha sanaa cha Nyota toka mjini Mbeya kitakacho onesha sarakasi, maigizo na ngoma.

MWISHO

Friday, May 9, 2008

Posted by Unknown On 3:12 AM 1 comment
Mbozi Meteorite fell at Malengi hill, Ndolezi village of Mbozi district

Lake Ngozi, a crater at the top of Mt. Ngozi in Mbeya rural

A pottery is a business of lake Nyasa residents (Kisi tribe)


Site search

    More Text