Saturday, April 18, 2009

HOFU KWA MAALBINO

Posted by Unknown On 3:26 AM No comments
Wadau ni muda mrefu sikuwepo hewani tuungane tena.

Judith Msongole mlemavu wa ngozi (Albino) wa kijiji cha Chipaka wilayani Mbozi anaishi kwa hofu ya kuuliwa! jamani hapo sasa ni mambo!

Jamani uungwana uko wapi? Maisha ya albino yanapokuwa hatarini na hasa watu wanapojitokeza kuwatisha wazi wazi wakiwa na nia ya kuwadhuru na kupata viungo vyao. Sasa mama huyo anaishi kwa hofu, polisi nao wamechelewa kuchukua hatua za kumkamata mtuhumiwa sasa mabishano ni kati ya polisi na mume wa mlalamikaji.

Mkuu wa kituo anadai mlalamikaji hajaenda kumwona ilihali mume wa mlalamikaji anadai kwenda zaidi ya mara tatu polisi lakini wanajibiwa visivyo.

Viongozi chukueni hatua za kukomesha mauaji hayo.

Jakaya Kikwete chukua hatua zile alizochukua Mwalimu Nyerere kukomesha mauaji yaliyokuwa yanatokea Tukuyu hasa Ikuti kwa imani za kishirikina miaka ya sabini. Mbinu ile itasaidia, wachawi wote maarufu kama Manyafu walipitiwa na operesheni ile ambayo iliwahamishia Mafia na kuwekewa stop wasirudi mkoani Mbeya.

Hatuwezi kukuelekeza, bado unao maafisa walioshiriki operesheni ile tafadhali uwatumie japo kwa kiasi. Tuone waganga hao wakifanyia uganga huko uhamishoni ikiwezekana ni kuwakusanya pote walipo.
Pamoja na agizo la Waziri Mkuu Mh. Pinda kufuta leseni za waganga wa jadi bado waganga wanaendelea kutoa huduma kwa wateja huku wakiweka mabango yao barabarani hadharani.

Shiriki hapo ulipo kutokomeza mauaji ya albino.

0 comments:

Post a Comment

Thank you for reading the article

Site search

    More Text