Tuesday, August 5, 2014

Wakulima kazi kwelikweli

Posted by Unknown On 12:36 PM No comments

Pamoja na jitihada zinazofanywa na mkulima mmoja mmoja za kuzalisha mazao ya kilimo chakula na biashara bado mazingira yake ni magumu analima bila kuwa na uhakika wa soko. Bei zenyewe zinapangwa na wanunuzi halafu sisi wa mjini tunalaumu ughali wa chakula kumbe ni wanunuzi wa kati ndiyo wanalangua mazao hayo. Serikali iandae vema mazingira ya kuwa na soko la uhakika kupitia mamlaka zake au hata vyama vya wakulima (vikundi). 
Ushirika uliotarajia kusaidia kutatua matatizo ya soko leo hii ushirika ni marehemu na bila kutafuta chombo mbadala hali itaendelea kuwa mbaya. Serikali itenge fedha za ununuzi wa mazao yote na kuelekeza nguvu kama sera inavyotamka.

Serikali ikishindwa kumtafutia mkulima soko la mazao yake itawalazimu kudai kwa nguvu kwani mkulima hana likizo yaani sawa na yatima kwani yatima hadeki.


Mambo yalivyokuwa katika uwanja wa nanenane wa John Mwakangale juu ni vifaranga wa Malawi chini ni mkulima wa Tunduru akiwa katika banda lake akionesha muhogo babu kubwa.

Hapo juu ni madumu ya asali ya nyuki wakubwa ba wadogo karibuni

Maonesho haya hayakuacha kuonesha kuku kama ndege wa kukupa kipato na anaweza kufugwa na kaya maskini.
Hao kuku ni aina ya Kenya wanaitwa Kenbro Dr Mbwaga wa Uyole ndiye mfugaji wa kuku hao

Nanenane 2014 Kilimo ni Biashara

Posted by Unknown On 12:09 PM No comments
Maonesho ya kilimo, mifugo na ujasiriamali ni fursa pekee inayoonesha hisia za watanzania kuhusu matarajio yao kulinganisha na fursa zilizopo.

Watunga sera wamekuwa wakiwayumbisha wakulima kwa kutoa sera zisizotekelezeka na porojo nyingi. Ilipobuniwa kaulimbiu ya Kilimo kwanza wengi walikuwa na tumaini ya kuushinda umaskini wakidhani serikali ingekuja na mikakati kabambe ya utekelezaji wa kilimo kwanza kwa vitendo kumbe sivyo ilivyotokea.

Maenesho ya nanenane jijini Mbeya yamefana licha ya kukumbana na changamoto kadha wa kadha zinazojitokeza. Tumaini la wakulima walio wengi walitarajia sera imara zingewekwa ili kuwa na fursa kwa vyombo vya fedha kuchangia moja kwa moja katika kilimo.

serikali ibuni mikakati ya kuwakopesha wakulima hawa wadogo wajishughulishe na ujasiriamali utakaohusisha usindikaji wa mazao yao na kuyauza vizuri.

Kati ya mambo yaliyochekesha mwaka huu ni pale serikali inapojitangaza na kujigamba kuwa itaiuzia shehena ya mahindi Kenya takriban tani 50000, Tujiulize kuwa fursa iliyokuwepo inapotea kwa kuuza ghafi bila kusindika na kuyaongezea thamani huo ni upwagu.


Hilo ndiyo banda la maonesho la jiji la Mbeya linasema Kilimo ni Biashara.

Hilo ni kati ya mabanda machache yaliyoandaliwa

Hiyo ni bustani ya jiko imewekwa hapo kama shamba darasa kwa mtu asiye na eneo unaweza kufanya hivyo

Site search

    More Text